Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Na Arone Mpanduka

Chimbuko la bendi ya Maquis du Zaire kwa nchi ya Tanzania lilianzia mwaka 1973, wakati Franco Luambo Luanzo Makiadi akiwa na bendi yake ya T.P. OK. Jazz alikuja hapa nchini na akafanya onyesho kamambe katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam(sasa uwanja wa Uhuru).
Mwaka mmoja baadae wa 1972, bendi ya Maquis du Zaire, nayo ikaingia kwa mbwembwe na kuweka makazi yake ya kudumu katika jiji la Dar es Salaam.
Bendi hiyo Maquis du Zaire iliyotokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ikafia humu nchini miaka ya 1990.
Ilikuwa kivutio kikubwa kwa Watanzania na kuwapa hekaheka wanamuziki wa Tanzania katika miaka hiyo.
Kwa nchini Congo, bendi hiyo ilianza mwaka 1960, vijana wa wakati huo katika mji wa Kamina huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), waliungana na kuunda bendi yao, wakaiita Super Theo.
Bendi hiyo ilikuwa ikitoa burudani tosha kwa wapenzi wa muziki wa mji huo wa Kamina na vitongoji vinavyouzunguka mji huo. Baadae wakaibadilisha majina na bendi ikawa Super Gabby. Lakini uongozi wa Super Gabby ulitaka kuleta mageuzi katika muziki mwaka 1972, walipobadilisha majina rasmi na kuwa Maquis du Zaire.
Mwaka huo huo bendi hiyo iliingia hapa Tanzania wakipitia nchini Uganda.
Walipofika katika jiji la Dar es Salaam, walipata mkataba wa kupiga muziki katika ukumbi wa Mikumi Tours, uliokuwa maeneo la Tazara Buguruni, jijini Dar es Salaam.
Baada ya kumaliza mkataba wao, waliondoka wakaenda kupiga muziki katika Klabu ya Hunters kwa kipindi kifupi.
Kisha viongozi wa bendi hiyo wakafanya mazungumzo na mfanyabiashara Hugo Kisima, aliyekuwa akimiliki ukumbi wa Safari Resort, maeneo ya Kimara, jijini Dar es Salaam. Wakaanza kupiga muziki kwa mkataba na mfanyabiashara huyo.
Februari 1977 viongozi wa bendi hiyo ya Maquis du Zaire, waliamua kukiongezea nguvu kikosi chao. Hivyo walimtuma Tchibangu Katayi ‘Mzee Paul’ aliyekuwa mwanamuziki wa bendi ya Maquis du Zaire.
Pia alikuwa mmoja kati ya viongozi wa bendi hiyo.Mzee Paul aliwachukua baadhi ya wanamuziki ili kuja nao Tanzania kuongeza nguvu katika bendi ya Maquis du Zaire.
‘Mzee Paul’ alibahatika kuwachukua wanamuziki akina Kikumbi Mwanza Mpango, au ‘King Kiki’, mtunzi na mwimbaji, Kanku Kelly kwa upande wa tarumbeta., Ilunga Banza ‘Mchafu’, aliyekuwa akiungurumisha gitaa la besi, Mutombo Sozy aliyekuwa akizicharanga ‘drums’, na mnenguaji Ngalula Tshiandanda.
Wakati huo Maquis du Zaire walikuwa wakicheza muziki wakitumia mtindo wa ‘Chakula Kapombe’, ambao kwa Watanzania ulikuwa mpya, na ukapendwa mno na mashabiki.
Kufika kwa wanamuziki hao, kulileta changamoto kubwa katika muziki. Tungo nzuri za Kikumbi Mwanza Mpango ‘King Kiki’, zilikuwa chachu masikioni mwa wapenzi wa muziki wa dansi. Kiki pia yaelezwa kuwa ndiye aliyeleta Mapinduzi makubwa ya muziki hapa nchini Tanzania.
Maquis du Zaire wakaazisha mtindo mwingine wa ‘Kamanyola’, uliowapagaisha wapenzi na wadau toka pembe zote za jiji la Dar es Salaam.
Mwishoni mwa 1977, Marquis du Zaire walimaliza mkataba kwa Hugo Kisima, wakaondoka.Bahati nyingine ikawadondokea tena baada ya kuingia mkataba mwingine wa kupiga muziki kwa mzee Makao, aliyekuwa akimiliki ukumbi wa Savannah, maeneo ya Ubungo.Wakiwa Savannah, walianzisha mitindo ya ‘Sanifu’, na ‘Ogelea piga mbizi’.
Lakini ukumbi huo ukabadilishwa jina ukaitwa White House. Ikumbukwe kwamba Maquis pia ilikuwa ikipiga kwenye ukumbi wa Mpakani, maeneo ya Mwenge.Mwishoni mwa mwaka 1978, Maquis du Zaire  waliamua kuimarisha tena kikosi chao kwa kuwaleta wanamuziki wengine wapya kutoka DRC.Iliwaleta akina Kabeya Badu, Kalala Mbwebwe, Ngoyi Mubenga na Khatibu Iteyi Iteyi.
Bendi hiyo ilikuwa ikiongozwa na wanahisa akina Chinyama Chiyaza ‘Chichi’, Chibangu Katayi ‘Mzee Paul’, Chimbwiza Mbangu Nguza au ‘Nguza Vicking’, Mutombo Lufungula ‘Audax’ na Mbuya Makonga ‘Adios’.
Chini ya uongozi huo, katika miaka ya 1980 mafanikio makubwa yalionekana, mojawapo ni lile la kuanzisha Kampuni iliyofahamika kama Orchestra Maquis Company (OMACO).
Kampuni hiyo iliweza kumiliki shamba la matunda, wakalima kwa kutumia trekta zao maeneo ya Mbezi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Mazao yao walikuwa wakiyapeleka na kuuza katika Soko Kuu la Kariakoo jijini Dar es Salaam.OMACO pia ilimiliki mradi mwingine wa viwanja tisa na nyumba kadhaa, maeneo ya Sinza, jijini Dar es Salaam.
Kwa wakati huo, watu wengi hawakuwa na haja ya kuchukua teksi kurudi nyumbani, kwani muziki wa Maquis du Zaire ulikuwa unarindima hadi alfajiri. Muda ambao mabasi ya UDA ya Ikarus yalikuwa yameanza kazi. Wakati huo hazikuwepo ‘Dala dala’, Bajaji wala Pikipiki kwa maana ya Bodaboda.
Hata hivyo, baadae bendi hiyo ilianza kufa taratibu kufuatia baadhi ya wanamuziki kuondoka kwenda kutafuta maisha sehemu nyingine, na wengine kusahindwa kufanya kazi hiyo kutokana na umri kuwa mkubwa, na magonjwa ya hapa na pale.
Mwanzoni mwa miaka ya 1990, bendi ilipotea kabisa na kuacha historia ya kipekee.
Baadhi ya nyimbo za Marquis du Zaire zilizovuma kwa uzuri na utamu wake ni ‘Ni Wewe Pekee; Makumbele; Kalubandika; na Promotion’.
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

WAWATA watikisa Visiga

September 02, 2022

KIBAHA

Na Mathayo Kijazi

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi amewataka Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA), na waamini wote kutambua kwamba wanapomsifu Mtakatifu Agustino, wanapaswa pia kumshukuru Mama yake mzazi Mtakatifu Monica.
Askofu Ruwa’ichi aliyasema hayo wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Kilele cha Jubilei ya Miaka 50 ya Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA) Kijimbo, katika Kumbukumbu ya Mtakatifu Monica, iliyofanyika katika Seminari Ndogo ya Mtakatifu Maria, Visiga, jimboni humo.
“Tunaadhimisha mambo kadhaa, kwanza kabisa tunawamkumbuka WAWATA, na hususan Mtakatifu Monica, mama yake Mtakatifu Agustino. Huyu ni mama wa mfano, mama aliyetukuka, mama wa kuigwa. Mama huyu alizaliwa mwaka 331 katika Bara la Afrika, huko Afrika ya Kaskazini,” alisema Askofu Mkuu, na kuongeza,
“Alizaliwa na kulelewa vizuri katika familia ya Kikristo, akajenga na kustawisha fadhila zilizo njema; fadhila ya Imani; fadhila ya mapendo; fadhila ya huruma na fadhila za kimama. Tumtukuze Mungu kwa zawadi ya Mama huyu kutoka Bara la Afrika,” alisema Askofu Mkuu Ruwa’ichi.
Askofu Ruwa’ichi aliwapongeza WAWATA kwa kuendelea kusimama imara na kwa kujitolea kwao katika shughuli mbalimbali za Kanisa, huku akiwasihi kufahamu kwamba wao ni zawadi ya Mungu kwa Kanisa na Ulimwengu.
Askofu Mkuu Ruwa’ichi alimshukuru Mungu kwa utume unaofanywa na akinamama hao, hasa kuwalea Vijana wa Seminari ya Visiga, akimwomba Mungu awazidishie neema na baraka zake, ili utume wao uendelee kustawi, na kuutukuza ukuu wa Mungu.
Askofu Ruwa’ichi aliwasihi WAWATA kutafakari kwamba wao ni baraka kutoka kwa Mungu, kwa uwepo wao wa Miaka 50 sasa, kwani Utume wa Wanaume Wakatoliki (UWAKA), hata miaka 30 bado hawajafikisha, huku akiwasihi akinamama hao kumshukuru Mungu kwa mema yote anayowajalia.
Aidha, aliwaasa WAWATA kuendelea kubaki kuwa Wakristo Wakatoliki wazuri, hata katika Kanisa la nyumbani, kwa kusimama imara na kuwa mama bora, hata katika familia zao.
Kwa upande wao, Maaskofu Wasaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu na Mhashamu Stephano Musomba, waliwapongeza WAWATA kwa kuadhimisha Jubilei yao ya Miaka 50, na kwa kazi nzuri ya utume wanaoendelea nao kuufanya jimboni humo.
Naye, Mwenyekiti wa Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA), Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Stella Rwegasira aliwashukuru waamini wote walioshiriki Adhimisho hilo.
Aidha, Catherine Mwingira, Katibu wa WAWATA Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam alisema kuwa wanamshukuru Mungu kwa kufikisha Miaka 50 tangu chama hicho cha Kitume kuanzishwe na waasisi wao, huku akisema kuwa yamefanyika mengi mazuri tangu kuanzishwa kwa chama hicho hadi sasa.
Chama cha Kitume cha Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA), kilianzishwa rasmi mwaka 1972.

Nairobi, Kenya
Mwendesha baiskeli wa Kenya Suleiman Kangangi amefariki dunia kufuatia ajali ya mwendo kasi katika mbio za magari nchini Marekani siku ya Jumamosi.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 ambaye alikuwa akishiriki mbio za changarawe za Overland huko Vermont, shindano la kilomita 59 la barabara za udongo, likijumuisha takriban futi 7,000 za kupanda.
Kangangi alimaliza wa tatu katika Tour of Rwanda mwaka wa 2017 alipokuwa akikimbilia timu ya UCI Continental ya Ujerumani, Bike Aid, kabla ya kubadili mbio za changarawe.
Kwa upande wake Rachel Ruto, mke wa rais mteule William Ruto wa Kenya, alichapisha kwenye Twitter, “Sote tutamkosa kama mtu binafsi. Kenya imepoteza bingwa. Pumzika kwa amani Sule”.
Nayo taarifa ya klabu yake ilisema, “Sule ni nahodha wetu, rafiki, kaka. Yeye pia ni baba, mume na mwana”.

Kamati ya Uongozi wa Kitaifa ya Kushughulikia Mambo ya Kitume iliyoteuliwa na Baraza la Maaskofu Katoliki nchini Ethiopia, ikiwa katika picha ya pamoja.

ADDIS ABABA, Ethiopia

Baraza la Maskofu Katoliki nchini Ethiopia limeunda Kamati ya uongozi Kitaifa, ili kushughulikia changamoto mbalimbali za Kitume.
Maaskofu hao wamepitia masuala msingi ya Kitume ya Kanisa, fursa na changamoto katika mkutano wao wa kawaida wa 53, na kuunda Kamati ya Uongozi ya Kitaifa itakayofanyia kazi maandalizi ya Mpango Mkakati wa Miaka 10, ili changamoto zilizojitokeza wakati wa mkutano huo, ziweze kutatuliwa ipasavyo.
Kamati ya uongozi ya Taifa itaongozwa na Katibu Mkuu Mchungaji Abba Teshome Fikre, na itakuwa na wajumbe 10 wakiwemo Naibu Katibu Mkuu, maafisa na wakuu wa CMRS, na Mshauri wa ndani.
Kamati ya kitaifa tayari imeanza kazi yake ya kujadili Mchakato wa Mpango Mkakati, kuandaa mikakati ya utekelezaji na jukwaa la awali la uhamasishaji. Kwa kuzingatia hili katika wiki chache zilizopita, kamati imeandaa Mpango Kazi wa Miezi Sita ijayo.
Kuanzia Agosti 10 hadi 13, awamu ya kwanza ya kazi imekuwa ziara katika Majimbo mbalimbali, na maandalizi ya mpango wa kina yamefanyika katika Majimbo sita, ambayo ni pamoja na Jimbo Kuu Katoliki la Addis Ababa, Vikariati ya Meki, Jimbo Katoliki la Kitume la Vazi, Vikariati za Hawasa, Sodo, Hossana, Jimma-Bonga, na Eparchy ya Emdibir.
Katika mchakato huo, majadiliano mbalimbali yalifanywa na Maaskofu na viongozi husika kuhusu Mpango Mkakati huo.
Baadhi ya ajenda zilizoonyeshwa katika mjadala ni pamoja na Asili ya Mpango Mkakati wa kina wa Kanisa; Umuhimu wa Mpango Mkakati wa Miaka 10; Mchakato na Changamoto za Sasa za Huduma ya Dayosisi; Wajumbe wa Kamati ya uongozi ya dayosisi wakishirikiana na kamati ya Taifa.
Kwa kuongezea, mafunzo mafupi kuhusu itifaki za mawasiliano na jukwaa pepe, yalitolewa ili mawasiliano ya kazi zijazo yawe na ufanisi.
Majadiliano mengine yatafanyika katika maeneo ya Eparchy ya Bahirdar-Dessie, Vicariate ya Nekemet, na Dayosisi ya Gambella, na wawakilishi wa makuhani wa Eparchy of Adigrat watafanya mkutano huko Addis Ababa.
Mpango Mkakati wa Kanisa nzima ni mojawapo ya maelekezo ya kazi yanayofuata yaliyoamuliwa na Baraza la Maaskofu, Mpango Mkakati wa Miaka 10 wa Kanisa utatayarishwa kwa kuzingatia maono ya pamoja ya Kanisa, kwa kuzingatia huduma ya kichungaji, maendeleo ya kijamii. na maelekezo ya kiutawala ya Kanisa.
Mpango wa miaka 10, unatathmini mipango ya awali iliyofanywa na taasisi za Kanisa, pamoja na ile ambayo imeanzishwa na inayotekelezwa. Muda mfupi wa mipango mkakati, changamoto katika utekelezaji na ukosefu wa tathmini kwa wakati, ulielezwa kuwa sababu kuu za kutotekelezwa.
Kamati ya Uongozi iligawa Mpango Mkakati katika awamu nne za utekelezaji, na kuweka ukomo wa muda kwa kila moja. Hatimaye, Mpango Mkakati unalenga Mashirika ya Kanisa kufanya kazi pamoja kwa ajili ya maono ya pamoja ambayo yanasimamia utume na maadili ya Kanisa Katoliki.

GULU, Uganda
Maandalizi ya kutangazwa Padri Joseph Ambrozoli kuwa Mwenyeheri yanaendelea vizuri, tukio litakalofanyika wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu itakayofanyika Jimbo Kuu Katoliki la Gulu, Uganda Novemba 20, mwaka huu.
Mchungaji John Baptist Odama wa Jimbo Kuu Katoliki la Gulu alisema kuwa Kamati Kuu ya Maandalizi (COC) yenye kamati ndogo 16 imeundwa, na wote wanafanya kazi ya kuona jinsi ya kuwapokea watu watakaokuja kuhudhuria ibada hiyo.

Page 1 of 3